2014-01-08 10:19:52

Mapigano ya Kikabila nchini Nigeria yasababisha vifo vya watu zaidi ya 40


Mapema juma hili watu zaidi ya arobaini wameuwawa kikatiliki, wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto huko Plateau na Kaduna, nchini Nigeria. Taarifa zinaonesha kwamba, haya ni mapigano ya kikabila yanayoendeshwa na Kabila la Fulani. Mapigano hayo yamepelekea nyumba na mifugo kadhaa kuchomwa moto!

Taarifa inaonesha kwamba, askari wanne waliokuwa wanarudi makwao baada ya kumaliza zamu yao ya ulinzi kwenye Benki Wilayani Rigasa walivamiwa na kuuwawa kikatili. Wachunguzi wa mambo wanasema, haya ni mapigano kati ya wafugaji wanaotafuta maeneo ya kulishia na kunywesha mifugo yao pamoja na wakulima wanaotafuta maeneo mazuri zaidi ya kilimo.

Mapigano kati ya kabila la Wafulani na Watarok, katika kipindi cha kuanzia mwaka 1992 hadi Mwaka 2013 yamesababisha zaidi ya wananchi elfu kumi kuuwawa kikatili huko Plateau na Kaduna, Nigeria.







All the contents on this site are copyrighted ©.