Papa Francisko, Jumapili, alitangaza kwamba ana mpango wa kufanya hija Nchi Takatifu
mwezi Mei mwaka huu. Tamko hili amelitoa ikiwa imepita siku moja tu, baada ya kupita
kumbukumbu ya miaka 50, tangu Khalifa wa mtume Petro , Papa Paulo VI, kufanya ziara
ya kihistoria ya kwanza , nje ya Italia, kutembelea maeneo Matakatifu mjini Bethlehemu
, Yerusalemu na Nazareth - Januari 4, 1964. Ziara hii ya kwanza nje ya Italia
ya Papa Paulo VI, ilifungulia mlango wa safari zingine, hatimaye kutembelea mabara
sita, ikiandika pia historia ya kwanza ya Mkuu wa Kanisa la Ulimwengu , Baba Mtakatifu
na Askofu wa Roma, kutumia usafiri wa ndege kwa mara ya kwanza. Historia inaonyesha
Hija hiyo ya kwanza ya Papa Paulo VI, pia iliweka alama ya mabadiliko ya msingi katika
mahusiano kati ya Kanisa Katoliki na Kanisa la Ki-Orthodosi ambamo Papa Paul VI
alikutana na mkuu wa Kanisa la Kiothodosi wakati huo, Patriaki wa Kiekumeni wa Constantinople,
Mwenye Heri Athenagoras I, katika bustani ya Mizeituni ya Yerusalemu . Kukutana
kwao kuliweza kuondoa vikwazo vilivyo kuwepo, kwa pande zote mbili, baada ya utengano
wa Makanisa ya Mashariki na Magharibi, tangu upinzani wa mwaka 1054. Papa Fransciko
Jumapili akizungumza na mahujaji waliojitosa katika hali mbaya ya hewa na kwenda kusali
pamoja nae sala ya Malaika wa Bwana na kumsikiliza , alisema , katika furaha ya
msimu huu wa noel, napenda kutangaza kwamba kuanzia Mei 24-26 ijayo , Mungu akipenda,
nitafanya hija katika Nchi Takatifu. Baba Mtakatifu alitaja lengo kuu la hija hii
yake, ni kushiriki katika kumbukumbu ya kutimia miaka 50 tangu Papa Papa Paulo VI
na Patriaki Athenagoras , walipokutana mnamo Januari 5, 1964. Na kwamba, anapanga
kutembelea miji ya Amman, Bethlehemu na Yerusalemu. Pia kwamba alipenda kushiriki
katika Mkutano wa kiekumeni , utakao fanyika katika Kanisa la Kaburi Takatifu na hudhuriwa
na wawakilishi wa Makanisa ya Kikristo ya Yerusalemu , pamoja na Patriaki Bartholomew
I wa Constantinople. Papa alimalizia ujumbe huo kwa kuomba sala za waaamini zimsindikize
katika nia na Hija hii."
Jumapili hiyo, Kabla ya Sala ya Malaika wa Bwana,
Papa Francisko alielezea jinsi sherehe za Noel, zinavyonyesha upendo mkubwa Mungu
alio nao kwa binadamu. Na kwamba kila adhimisho la kuzaliwa kwa Yesu duniani ni adhimisho
jipya, kwa ajili ya dunia kufanywa upya. Mungu , alisema, daima yupo tayari kuwalea
waume kwa wake, na kuutakatifu ulimwengu dhii ya dhambi , na Yesu daima hachoki kuwa
nasi na hakomi kutujalia neema yake ya kuokoa. Papa alikamilisha hotuba yake kwa
kuwashukuru wote waliomtumia salaam za matashi mema wakati wa Noel na mwaka mpya,
na kwa moyo wao wa kufiki kumsikiliza licha ya hali mbaya ya hewa.
Ziara
ya Papa Paulo VI, kutembelea Nchi Takatifu 1964, ilifuatiwa na ziara ya Papa Yohane
Paul II, wakati wa Jubilee mwaka 2000. Ziara hii ilichukuliwa katika mitazamo yote
miwili, kama binafsi, na pia kuwa hija ya kiroho katika eneo lenye mizizi ya imani
ya Kikristu , na pia kama ziara ya kidiplomasia iliyolenga kuimarisha maridhiano kati
ya Wakristo, Waislamu na Wayahudi wanaoishi Mashariki ya Kati.
Katika ziara
hiyo , kati ya picha za kukumbukwa, ni wakati ambapo Papa Yohane Paul II, alipotolea
sala zake katika jadi ya kiyahudi ya kuomboleza katika ukuta wa Yerusalem na kuacha
karatasi ya sala katika moja ya nyufa za ukuta huo. Iliwashangaza wengi kwamba, Papa
Yohane Paulo katika karatasi ya sala hiyo, aliomba msamaha wa Mungu kwa ajili ya dhambi
za Wakaristu dhidi ya Wayahudi.
Papa Benedict XVI nae alifuata nyayo za watangulizi
wake, na kutembelea Yerusalemu Mei 2009. Na kati ya maeneo mengine aliyozuru ni Mnara
wa kumbukumbu ya mauaji wa kinyama dhdi ya wayahudi, mnara wa Yad Vashem, Ambako
pia alikutana na waathirika wamadhulumu ya kinyama yaliyofanywa na maaskari wa Nazi.
Papa Benedikto XVI, mahali hapo alitoa wito na ahadi ya Kanisa kusaidia kuhakikisha
kwamba, chuki dhidi ya Wayahudi, kamwe isiruhusiwe kuwepo tena duniani.