Padre Georges Vandenbeusch, mwenye umri wa miaka 42 aliyekuwa ametekwa nyara na watu
waliokuwa na silaha hapo tarehe 14 Novemba 2013 wakati akitoa huduma kwenye Parokia
ya Nguetchewe, Kaskazini mwa Cameroon, ameachiliwa huru, mwishoni mwa mwaka 2013.
Habari hizi zimethibitishwa na Rais Francois Hollande wa Ufaransa ambaye anasema kwamba,
hali ya Padre Georges ni njema.
Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican
amepokea habari hizi kwa moyo wa furaha na shukrani na anawaalika waamini na watu
wenye mapenzi mema kuendelea kusali na kuwaombea watu mbali mbali waliotekwa njara
na hadi sasa hawajulikani mahali waliko.