Kamishna wa Polisi Ernest Mangu ateuliwa kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete Jumatatu, Desemba 30,
2013, amemteua Kamishna wa Polisi Ernest Mangu kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini
Tanzania. Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue inasema
kuwa Kamishna Mangu anachukua nafasi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini anayestaafu,
Saidi Mwema.
Kabla ya uteuzi wake unaoanza Januari Mosi, 2014, Kamishna Mangu
alikuwa Mkurugenzi wa Inteligensia ya Jinai (Director of Criminal Intelligence) katika
Jeshi la Polisi. Aidha, taarifa hiyo inasema kuwa Rais Kikwete amemteua Kamishna Abdulrahman
Kaniki kuwa Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi, ambayo ni nafasi mpya katika muundo wa
sasa wa Jeshi la Polisi. Kabla ya uteuzi wake, Kamishna Kaniki alikuwa Kamishna wa
Uchunguzi wa Kijinai (Commissioner for Forensic Investigations).