Jichoteeni amani na furaha ya ndani kutoka kwa Yesu
Mama Kanisa anapojiandaa kuadhimisha Siku kuu ya Bikira Maria Mama wa Mungu sanjari
na Siku ya 47 ya Kuombea amani duniani, Baba Mtakatifu Francisko, anawaalika watumiaji
wa mitandao ya kijamii kutoka katika Pango la Mtoto Yesu, kujichotea furaha na amani
inayoletwa na Yesu Kristo.