2013-12-31 12:21:01

Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya Bikira Maria Mama wa Mungu na Siku ya Kuombea Amani Duniani kwa mwaka 2014


Baba Mtakatifu Francisko, tarehe Mosi Januari 2014 anatarajiwa kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican kwa ajili ya Sherehe ya Bikira Maria Mama wa Mungu. Hizi ni kati ya sherehe kubwa za Bikira Maria zinazoadhimishwa na Kanisa katika Kipindi cha Mwaka sanjari na Siku ya Kuombea Amani Duniani.

Ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko kwa Mwaka 2014 unaongozwa na kauli mbiu "Udugu ni msingi na njia ya amani" mafundisho msingi ya Kanisa kuhusu masuala ya kijamii, kama sehemu ya mchakato wa kudumisha haki, amani na maendeleo endelevu.

Udugu ni jambo muhimu sana katika mapambano dhidi ya umaskini, ujinga na maradhi. Udugu unazima vita na madhara yake; upambana kufa na kupona na rushwa, ufisadi na uhalifu wa makundi. Udugu unalinda na kutunza mazingira.







All the contents on this site are copyrighted ©.