2013-12-27 14:48:07

Kardinali Ouellet asema, mwaka 2013 umekuwa ni mwaka wa kihistoria kwa Kanisa.


Katika mwaka huu tunao elekea kuufunga, kwa hakika umekuwa ni mwaka wa kipekee katika maisha ya Kanisa, na hasa kwa tukio jipya la kihistoria la kustaafu katika kiti cha Petro, Papa Benedikto XV1, na kuchaguliwa kwa mrithi wake Papa Francisko. Ni maoni ya Kardinali Marc Ouellet , Mkuu Decania ya Maaskofu, wakati akihojiwa na Hèlène Destombes wa Radio Vatican, juu ya kustaafu kwa Papa Benedikto XV1.

Kardinali Ouellet analichukulia tukio la kujiuzuru kwa Papa Benedikto XV1, kuwa ni tukio kubwa jipya katika historia ya kipindi kirefu kwa Kanisa. Kitendo kilicho shuhudia maana ya unyenyekevu na imani kubwa kwa Roho Mtakatifu, kwa ajili ya utendaji wa siku za usoni kwa Kanisa. Na hivyo tunapaswa kumshukuru Papa Benedikto XVI, kwa kufungua upya upeo wa macho, na fursa ya kuchaguliwa kwa Papa mpya Francisko.

Kardinali anaamini kwamba, kuna ni mwendelezo kwa yale yaliyoanzishwa na Papa Mstaafu Benedikto XVI, yanayo fanyiwa kazi na Papa Francisko. Na hivyo kwa tathmini ya mwaka 2013, inaonyesha kwamba, ulikuwa ni wakati wa mabadiliko makubwa katika historia ya Kanisa , katika mtazamo wa utendaji wa kichungaji kwa maongozi ya Papa Francisko.

Kardinali ametaja mageuzi hasa katika maisha ya Kiinjili, ambamo Papa Francisko, amekuwa akisisitiza mawasiliano mpya ya muumini kujiweka karibu zaidi na Mungu, bila ya kujali hali yao au itifaki yao, wote anawahimiza kumgeukia Mungu kama jambo la dharura. Na katika kufanya hivyo , anamtaka kila Askofu awe mchungaji mwema, wote kuwa wa mchungaji mwema, anayekaa daima karibu na wanakondoo wake, akiwachunga kwa moyo wa upendo mkuu na huruma , na akiwajaza zawadi ya faraja na matumaini mapya.

Na kwamba, katika mwaka huu 2013, katika mtazamo wa Papa Francisko, umetoa msisitizo mkubwa katika kujali maisha ya umma mzima wa dunia. Na huu ni mfumo mpya wa ajabu katika uinjilishaji. Papa amekuwa ni ishara ya ushawishi, katika hitaji la watu kujenga matumaini katika ubinadamu na kwamba Mungu hupatikana katika sura ya binadamu hasa mtu maskini na mnyonge. Hii ni habari njema kwa watu wote! tunapaswa kupokea ujumbe huo na kuufurahia.









All the contents on this site are copyrighted ©.