2013-12-26 11:22:35

Mwenyezi Mungu ulilisahau Bara la Afrika na Watu wake!


Baba Mtakatifu Francisko katika salam zake za Noeli kwa Mji wa Roma na Ulimwengu kwa ujumla, "Urbi et Orbi" amelikumbuka Bara la Afrika kwa namna ya pekee na kumwomba Yesu Mfalme wa Amani, kutolisahau wala kusahau mahangaiko ya wananchi wa Bara la Afrika.

Baba Mtakatifu amesali kwa ajili ya Nigeria ambako watu wasiokuwa na hatia wanaendelea kuteseka na kudhulumiwa. Amewakumbuka wale wote wanaoteseka kutokana na imani yao kwa Kristo na Kanisa lake. Katika sala zake, Baba Mtakatifu anaendelea kuwakumbuka wahamiaji, wakimbizi na watu wasiokuwa na makazi; hasa wale wanaoishi kwenye Kona ya Pembe ya Afrika na DRC.

Baba Mtakatifu anamwomba Mtoto Yesu asaidie mchakato wa upatanisho nchini Sudan ya Kusini, ambako vita na kinzani za kijamii zimekwisha sababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao. Vita anasema Baba Mtakatifu Francisko nchini Sudan ya Kusini inatishia amani, usalama na utulivu kati ya watu!







All the contents on this site are copyrighted ©.