2013-12-26 15:17:24

Katika adhimisho ya Siku Kuu ya Mtakatifu Stefano, Papa ahimiza kuwaombea wanaobaguliwa kidini.


Mama Kanisa akiadhimisha la Siku Kuu ya Mtakatifu Stefano, ambayo kijamii hujulikana kama "Boxing Day "Baba Mtakatifu Francisko, nyakati za adhuhuri kabla ya sala ya Malaika wa Bwana, aliwahutubia mahujaji na wageni waliokusanyika katika uwanja wa kanisa kuu wa Mtakatifu Petro.
Katika hotuba hiyo alieleza kuwa, maadhimisho ya Siku Kuu ya Noel, kiliturujia huendelezwa kwa muda wa siku nane. Na ni wakati wa furaha kubwa kwa watu wote wa Mungu ! Katika mwendelezo wa furaha hiyo, baada ya Siku Kuu ya kuzaliwa Kristu , Kiliturujia hufuatia Siku Kuu ya Mtakatifu Stefano , kama sehemu ya sikukuu hiyo. Mtakatifu Stefano , NI shahidi mfiadini wa kwanza wa Kanisa. Habari zake zimeandikwa katika Kitabu cha Matendo Mitume... Mtakatifu Stephano alikuwa ni mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu" ( 06:05 ). Pamoja nae pia waliteuliwa wengine sita kwa ajili ya kuhudumia wajane na maskini katika kanisa la kwanza wa Yerusalemu. Na aliuawa kwa kupigwa mawe nje ya ukuta wa mji wa Yesusalem. Papa amekifananisha kifo cha Stefano na kifo cha Yesu, kwamba wote waliowaombea msamaha wauaji wao.

Katika maelezo yake Papa amefafanua kwa nini Kanisa lina adhimisha Siku Kuu ya Mtakatifu Sptefano, ambayo kwa mtazamo wa haraka haraka mtu anapata fikira kama iko nje ya kipindi hiki cha kufurahia kuzaliwa kwa Bwana. Lakini kumbe katika kina cha imani, inahusiana na mwendeleo wa maisha. Amesema, Noel ni sherehe ya maisha mapya yenye kutupa hisia ya utulivu na amani , si kipindi cha kufkiria fujo na ghasia za kutisha. Lakini katika mtazamo wa mtazamo wa imani , Sikukuu ya Mtakatifu Stefano, ni mahali pake, katika maana ya ndani ya Noel. kwa kuwa katika kifo chandaniya Kristu huzaliwa maisha mapya. Katika vurugu mauaji hushindwa na hushindwa na upendo, na hivyo kifo hutoa maisha. Kanisa linaona katika majitoleo ya sadaka ya mashahidi wafiadijni, huzaliwa mbingu. Na hivyo kwa mtazamo huo, kumbe tunaisherhehea kuuawa kwa Mtakatifu Stefano inakuw ani Siku yake ya kuzaliwa upya, katika Kristo.Yesu hukibadili kifo cha wale wanaompenda na kumwamini kwa kuwapa maisha mapya.
Katika mauaji ya Stefano, mnaonyesha pia mapambano kati ya mema na mabaya, kati ya chuki na msamaha, kati ya upole na vurugu , ambayo ni hali halisi zilivyo kuwa , wakati wa Kifo cha Yesu Msalabani. Na hivyo kumbukumbu ya shahidi wa kwanza wa imani, hivyo, inafuta mara moja, sura ya noel ya uongo, ambayo haimo katika Injili.

Liturujia ya leo, inaturudisha katika maana ya kweli ya Umwilisho,inaunganisha Bethlehemu na Kalvari na kutukumbusha kwamba, wokovu ya Mungu, ni mapambano dhidi ya dhambi, ni kupita katika mlango mwembamba wa Msalaba. Hii ni njia ambayo Yesu aliweka wazi kwa wanafunzi wake , kama ilivyoshuhudiwa na Injili ya leo:nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu . Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokolewa "(Mt 10:22).

Hivyo, Baba Mtakatifu Francisko alihimiza kuomba hasa kwa ajili ya Wakristo , wanao baguliwa kwa sababu ya ushuhuda wao kwa Kristo na Injili. Na kutoa mwaliko wa kuwa karibu na ndugu, wake kwa waume, wale ambao, kama Mtakatifu Stefano, wanashutumiwa na kukabiliwa na unyanyasaji wa aina mbalimbali. Na hii inatokea hasa pale ambako, uhuru wa dini bado si wa uhakika au si kamilifu. Papa ameasa hili pia linaweza kutokea hata katika nchi zilizotia sahihi katika hati ya makubaliano ya kulinda uhuru wa dhamiri, na haki za binadamu, ambako waumini, na hasa Wakristo, bado wanakumbana na mapungufu katika uhuru wao na ubaguzi. Kwa Wakristo, hii si ajabu, kwa sababu Yesu alitabiri hilo kama fursa ya kuishuhudia imani.
Papa aliomba msaada wa maombezi ya Mama Bikira Maria Malkia wa Mashahidi atusaidie kukiishi kipindi hiki cha Noel, kwa mwamko wa imani na upendo kwa kuangaziwa na Mtakatifu Stefano na mashahidi wafia dini wa Kanisa.


Baada ya Sala ya Malaika wa Bwana, Papa alitoa salaam zake za matashi mema nabaraka kwa makundi mbalimbali zikiwemo familia kutoka Parokia mbalimbali za jimbo la Roma, na wale wote wanaofanya hija katika Pango la Noel, kumwona Mtoto Yesu, Maria na Yosef , waweze kutoa ahadi ya ukarimu wa upendo kwa mtu mwingine, ili ndani ya familia na jamii, watu waiishi hali ya hewa ya uelewa na udugu, kwa ajili ya manufaa ya wote.








All the contents on this site are copyrighted ©.