2013-12-23 09:37:25

Jumuiya ya Kimataifa inawataka viongozi wa Sudan ya Kusini kuanza majadiliano ili kurejesha amani na utulivu!


Rais Salva Kiir na aliyekuwa Makamu wa Rais Sudan ya Kusini Bwana Riek Machar wameamua kufanya mazungumzo yasiyokuwa na masharti kama njia ya kurudisha tena amani na utulivu Sudan ya Kusini ambayo hivi karibuni imejikuta ikitumbukia katika vita ya wenyewe kwa wenyewe na hivyo kusababisha maafa makubwa kwa watu!

Taarifa za kidiplomasia zinabainisha kwamba, viongozi hawa wawili ambao kwa sasa wanapingana ameamua kufuata ushauri uliotolewa na Mawaziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa kutoka Umoja wa Afrika. Rebecca Garang, mjane wa John Garang ameonesha nia ya kushiriki katika mazungumzo haya.

Jumuiya ya Kimataifa inawataka viongoni wa Sudan ya Kusini wanaopinga kuonesha utashi wa kisiasa kwa kusitisha mapigano, ili amani na utulivu viweze kutawala tena. Machafuko ya kisiasa na kijamii nchini Sudan ya Kusini yanatishia amani na usalama Ukanda wa Afrika Mashariki na kati!







All the contents on this site are copyrighted ©.