Siku kuu ya Noeli, Yesu apewe kipaumbele cha kwanza
Baba Mtakatifu Francisko anawaalika waamini kwa namna ya pekee katika Siku kuu ya
Noeli kuhakikisha kwamba, wanaiadhimisha mintarafu changamoto za Kiinjili, kwa kutoa
kipaumbele cha kwanza kwa Yesu katika maisha na vipaumbele vyao.
Baba Mtakatifu
Francisko, Jumamosi asubuhi anatarajiwa kukutana na Makardinali, Maaskofu na wasaidizi
wake wa karibu kama sehemu ya utamaduni wa kutakiana kheri na matashi mema wakati
wa Maadhimisho ya Siku kuu ya Noeli.