Kardinali Thèodore Adrien Sarr, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dakar, Senegal, hivi karibuni
amewataka waamini na watu wenye mapenzi mema kujisadaikisha zaidi, ili kukamilisha
ujenzi wa Madhabahu ya Jimbo yaliyowekwa chini ya usimamizi wa Mtakatifu Paul de Grand
Yoff.
Anasema, inasikitisha kuona kwamba, waamini wanakuwa wachoyo na kukosa
ukarimu kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya Kanisa mahalia. Kila mwamini akijitosa
kimasomaso kuchangia ujenzi wa Kanisa, mafanikio makubwa yanaweza kuonekana mara moja.
Ustawi na maendeleo ya Kanisa mahalia ni dhamana inayopaswa kutekelezwa na waamini
wenyewe.
Kardinali Sarr anawashukuru waamini ambao wanaendelea kuchangia kwa
hali na mali ili kufanikisha ujenzi wa Kanisa, ulioanza kunako Mwaka 2000, mara tu
alipoteuliwa kuwa Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dakar, Senegal. Madhabahu haya ni muhimu
sana katika mikakati ya shughuli za kichungaji, Jimbo kuu la Dakar, Senegal. Hapa
kuna Kanisa la Parokia, ujenzi wa Chuo kikuu; Chuo cha ufundi na uuguzi.
Kardinali
Sarr anasema mradi huu umepanuliwa ili kuhakikisha kwamba, Jimbo kuula Dakar, Senegal
linapata mahali ambapo waamini wanaweza kushiriki kwa idadi kubwa kwani Kanisa kuu
la Jimbo kuu la Dakar kwa sasa ni dogo na haliwezi kukidhi mahitaji ya ongezeko kubwa
ya idadi ya waamini wanaoshiriki katika Ibada mbali mbali. Gharama za ujenzi wote
hadi kukamilika zinakadiriwa kuwa ni Euro millioni 4. 5