Papa Francisko aridhia uteuzi wa Kardinali Angelo Amato
Baba Mtakatifu Francisko ameridhia uteuzi wa Kardinali Angelo Amato, Mwenyekiti wa
Baraza la Kipapa la kuwatangaza waamini kuwa wenyeheri na watakatifu. Ameridhia pia
wajumbe waliokuwa wanaunda Baraza hili sanjari na kuwateua wajumbe wengine, ili kuimarisha
utume na dhamana ya Baraza hili la Kipapa.