Mchakato wa maboresho ya huduma zinazotolewa na vyombo vya mawasiliano ya jamii vya
Vatican
Tume ya Kipapa inayopembua kuhusu shughuli za kiuchumi na kiutawala mjini Vatican
kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za zabuni, imeikabidhi Kampuni ya McKinsey
kufanya upembuzi wa kina kuhusiana na vyombo mbali mbali vya mawasiliano ya Jamii
vinavyomilikiwa na kuendeshwa na Vatican, ili kutoa ushauri unaopania kufanya maboresho
ya huduma zinazotolewa na vyombo hivi katika ulimwengu wa kisasa.
Ushauri
wa Kampuni hii utaisaidia Tume ya Kipapa kufanya maboresho zaidi, ili kuviwezesha
vyombo hivi kutoa viwango na ubora wa kimataifa; ushauri ambao baadaye unaweza kufanyiwa
kazi na Baba Mtakatifu katika mchakato wa mabadiliko yanayokusudiwa na Kanisa kwa
sasa.