2013-12-19 08:14:28

Biashara haramu ya dawa za kulevya inavyoichafua sura ya Tanzania!


Dr. James Msekela Balozi wa Tanzania nchini Italia na Mwakilishi wa Tanzania kwenye Mashirika ya Umoja wa Mataifa yenye makao yake makuu mjini Roma anasema, kwa masikitiko lakini kwa ujasiri mkubwa kwamba Tanzania kwa siku za hivi karibuni imechafuka kwenye ramani ya kimataifa kutokana na baadhi ya watanzania kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya. RealAudioMP3

Dr. Msekela ameyasema hayo hivi karibuni katika Maadhimisho ya Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania mjini Roma. Amewakumbusha viongozi wa kidini kwamba, wanayo dhamana ya kimaadili kuwasaidia watu wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya, kwa kuwaonesha njia mbadala ya kutafuta maisha, hasa wanapokuwa ugenini. Njia za mkato zinawatumbukiza watu katika majanga na maafa!

Anasema, inatia aibu na inakera sana, kumbe kuna haja kwa watanzania wote katika ujumla wao,. kushirikiana kwa pamoja kupambana na biashara pamoja na matumizi haramu ya dawa za kulevya.

Dr. Msekela amewasihi viongozi wa kidini kuendelea kuiombea Tanzania hasa baada ya kupata uhuru, kwani uhuru ni kazi na dhamana ambayo inapaswa kufanyiwa kazi. Uingereza ilimkabidhi Mwalimu J. K. Nyerere nchi kwa vile waliamini kwamba, Nchi itakuwa kwenye mikono salama kutokana uadilifu, umahiri, umakini, lakini zaidi kutokana Mwalimu kuwa ni Mchamungu.







All the contents on this site are copyrighted ©.