Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anabainisha
kwamba, ni vigumu kuweza kufikiri kuhusu Mashariki ya Kati bila ya uwepo wa Wakristo.
Baba Mtakatifu anawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema kusali kwa
ajili ya kuombea amani huko Mashariki ya Kati.