Papa awashukuru wajumbe wa Mfuko wa Domenico Tardini kwa kusimama kidete kulinda na
kutetea utu na heshima ya binadamu!
Baba Mtakatifu Francisko, Jumapili iliyopita, tarehe 15 Desemba 2013, alikutana na
kuzungumza na wajumbe wa Jumuiya ya "Domenico Tardini dil Villa Nazareth" walioshiriki
katika Ibada ya Misa takatifu kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican.
Amemshukuru kwa namna ya pekee Kardinali Achille Silvestrini, Rais wa Mfuko wa Jumuiya
ya Domenico Tardini, inayojielekeza zaidi katika kulinda na kutetea utu na heshima
ya binadamu.
Baba Mtakatifu amewataka wanajumuiya hawa kuhakikisha kwamba,
wanatumia vyema karama na vipaji walivyokirimiwa na Mwenyezi Mungu kwa mafao ya wengi
ndani ya Jamii. Hiki ni kielelezo cha mshikamano wa dhati ndani ya Kanisa na kwa
ajili ya Kanisa. Amewasihi kuendelea kumsindikiza katika sala na sadaka zao, ili aweze
kutekeleza kwa umakini mkubwa utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro.