Majembe mapya ya uongozi Umoja wa Watanzania wanaosoma Roma
Umoja wa wanafunzi wakatoliki watanzania wanaosoma mjini Roma, Jumapili iliyopita,
tarehe 15 Desemba 2013 wamechagua viongozi wapya, watakaooongoza Umoja huu kwa kipindi
cha Mwaka 2013- 2014. Uchaguzi huu umesimamiwa na Padre Dietrich Pendawazima, Makamu
mkuu wa Shirika la Waconsolata pamoja na Dr. James A. Msekela, Balozi wa Tanzania
nchini Italia na Mwakilishi wa Tanzania kwenye Mashirika ya Umoja wa Mataifa yenye
makao yake mjini Roma.
Waliochaguliwa
ni Padre Gaston Mkude kutoka Jimbo kuu la Dar es Salaam kuwa Mwenyekiti mpya. Wengine
ni Shemasi Romanus Wissa aliyechaguliwa kuwa Katibu. Sr. Regina Siyumbu amechaguliwa
kuwa mweka hazina; Padre Pambo Martini Mkorwe, OSB amechaguliwa kuwa kiongozi wa Ibada
na Padre Clement Kihiyo amechaguliwa kuwa ni Mkutubi mkuu wa Nyaraka za watanzania
wanaosoma Roma.
Balozi Msekela amewashukuru na kuwapongeza viongozi waliomaliza
muda wao kwa kazi kubwa waliyoifanya katika kuwahudumia watanzania wenzao. Ni matumaini
yake kwamba, viongozi wapya wataendeleza na kuboresha huduma hii makini kwa ajili
ya mafao, ustawi na maendeleo ya watanzania na Kanisa katika ujumla wake.