Imani ni fadhila ya Kimungu ambayo kwayo tunamsadiki Mungu na kila kitu alichokisema
na alichotufunulia, na ambacho Kanisa Takatifu latutaka tukisadiki, kwa sababu Yeye
ndiye Ukweli wenyewe. Kwa imani mwanadamu hujitoa nafsi yake yote kwa Mungu.
Ni
kwa sababu hiyo mwamini hutafuta kujua na kufanya mapenzi ya Mungu. Mwenye haki ataishi
kwa imani na imani. Na imani hai hutenda kazi kwa upendo.
Baba Mtakatifu Francisko
katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anasema, tumaini la Mkristo
ni kwamba: wakati ujao uko mikononi mwa Mwenyezi Mungu.