2013-12-13 15:49:33

Papa Francisko ala miaka 44 ya kuwa Padre.


13 Desemba ya mwaka 1969, miaka 44 iliyopita, historia ya maisha ya Jorge Mario Bergoglio ilifunua ukurasa mpya, baada ya kula kiapo cha kujiunga katika daraja Takatifu la Upadre, chini ya kanuni ya shirika la Kitawa la Wajesuiti.

Mkurugenzi wa Idara ya Maadili ya kitauhidi, katika Chuo Kikuu cha Kipapa Gregorian, Padre Miguel Yanez, Mjesuit , Mu-argentina, Mwenye kumfahamu Papa kwa ukaribu zaidi , katika kipindi cha miaka ya nyuma, katika mahojiano na Radio Vatican , ameyaeleza maisha ya Padre Bergoglio, kwamba, tangu kumfahamu , wakiwa nchini mwao, maisha yake ya Kipadre, daima alipenda kushirikiana na wengine katika yote, iwe maisha ya kijumuiya na kikanisa , Ibada za Misa,au kimasomo, na hata palipokuwa na nafasi za burudani, alishiriki vyema. Hizi ni kumbukumbu zilizobaki kwa wengi.

Padre Yanez amesema, Padre Begoglio tangu mwanzo alikuwa na mvuto kwa watu na alipenda kukutana na watu na kushirikishana nao mengi yakiwemo matatizo, hasa hali ngumu za kutatiza. Daima aliwadumisha watu katika kuwa na tumaini la kupata ufumbuzi kwa njia ya kushirikishana mawazo.

Na akirejea kuchaguliwa kwa Papa Francisko na gazeti la Times Magazine kuwa mtu mashuhuri wa mwaka, amesema , kuchaguliwa kwake kunatoa ujumbe, kwanza wa kumtakia mema, kwake yeye Papa Francesco ambaye siku za nyuma alijaribu kila njia kuviepa vyombo vya habari, maana alitenda si kwa kutafuta ufahali katika vyombo vya habari bali kw amoyo w aupndo wa ndani katika kuhudumia wengine. Alifanya mengi kimyakimya kisiri bila kutafuta makuu. Lakini kwa sasa amejikuta mbele ya vyombo hivyo na Huduma yake sasa si siri tena, maana anatazamwa na dunia zima. Na Kanisa linahitaji mtu kama huyu, kuufikisha ujumbe wa Injili kwa watu wote, kupitia njia zote. .








All the contents on this site are copyrighted ©.