2013-12-13 15:34:57

Papa : Wakristo wenye mzio na wahubiri daima ni wakosoaji, wenye kumfungia nje Roho Mtakatifu


Wakristo wenye kuwa na mzio(allergic) na wahubiri daima huwa na jambo la kukosoa. Lakini, katika hali halisi, ndani mwao wana woga fulani wa kumfungulia mlango Roho Mtakatifu. Ni watu wenye kuwa na wasiwasi, mashaka na huzuni ndani mwao. Papa Francisko alieleza wakati wa Ibada ya Misa, aliyo iongoza katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta mapema asubuhi ya Ijumaa hii Vatican..

Homilia ya Papa ikilenga katika somo la Injili ambamo Yesu analinganisha kizazi cha nyakati zake na watoto wanaowaita wengine kucheza pamoja, lakini wanakataa kuitikia wito huo kwa sababu hawajui kucheza na wengine kwa furaha, kwao hakuna lililo jema, ila wasiwasi na huzuni.
Papa amefafanua kwamba, watoto hao wanaokataa ni sawa na watu wasiopenda kujifunua kwa neno la Mungu, ambao kwao si hukataa kusikiliza ujumbe wa Neno lakini humkataa mjumbe mwenyewe, kama walivyo mkataa Yohane Mbatizaji, wakisema hali wala kucheza nao, wakimwita ni mwenda wazimu. Na pia walimkataa Yesu wakimwita ni mlevi, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi. Watu hao daima, walikuwa na sababu za kumkosoa mhubiri.

Papa amesema , Wakristo wa namna hii, wanasikitisha kwa sababu hawaaamini katika nguvu ya Roho Mtakatifu, hawaamini katika uhuru unaopatikana katika kusikiliza mahubiri, ambamo mna mafundisho na maonyo. na pia mna uhuru mwingi unaolipa kanisa nguvu za kusonga mbele. Hawa ni Wakristu wenye kuwa hofu za kufurahi na wengine, hofu katika kila jambo, hata usalama wao. Hili linasikitisha kwa sababu daima huwa na tabia ya kukosoa wahubiri wa ukweli, kwa sababu wanaogopa kufungua mlango kwa Roho Mtakatifu.
Papa alisema, tuombe kwa ajili yao, na tuombe pia kwa ajili yetu, ili kwamba pasiwe na Wakristo wa aina hii waliojaa huzuni,,wasiwasi na mashaka, wenye kukataa kumfungulia mlango Roho Mtakatifu. Ili waruhusu Roho Mtakatifu kuingia kwa uhuru,na kukaaa ndani mwao. Roho Mtakatifu anaye kuja kwetu kwa njia ya kashfa ya Mhubiri.








All the contents on this site are copyrighted ©.