2013-12-13 11:14:47

DRC na M23 watiliana sahihi mkataba wa amani


Katika Maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 50 ya Uhuru wa Kenya, Serikali ya DRC pamoja na Jeshi la M23, siku ya Alhamisi tarehe 12 Desemba 2013 wametiliana mkataba wa amani, tukio ambalo limeshuhudiwa na viongozi mbali mbali wa Serikali waliokuwa wanahudhuria Jubilee ya Miaka 50 ya Uhuru wa Kenya mjini Nairobi.

Taarifa hii imebainishwa na Bwana Manoa Eisipisu, msemaji wa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya. Ni matumaini ya wananchi wengi wa DRC kwamba, mkataba huu uliotiwa sahihi na wadau husika hautafungiwa kwenye makabati ofisini na watu wakaendelea kutwangana mitaani! Tukio hili limeshuhudiwa na Rais Joyce Banda kutoka Malawi ambaye pia ni Mwenyekiti SADC pamoja na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Nchi za Maziwa Makuu.

Viongozi watambue kwamba, wana dhamana ya kimaadili na kisheria kuhakikisha kwamba, wanatekeleza makubaliano haya kwa ajili ya mafao na ustawi wa wananchi wa DRC ambao kwa miaka mingi wameendelea kuteseka kutokana na vita pamoja na kinzani za kijamii na kisiasa.







All the contents on this site are copyrighted ©.