Wachunguzi wa masuala ya kivita wanasema, hali bado ni ngumu sana Jamhuri ya Watu
wa Afrika ya Kati. Milio ya risasi na milipuko ya mabomu inaendelea kusikika, vitendo
vinavyoendeshwa na Kikosi cha Seleka pamoja na wanajeshi ambao wameendelea kuwa waaminifu
kwa Rais Francois Bozize aliyeng'olewa madarakani Mwezi Machi 2013.
Kinzani
hizi za kivita zinakwamisha zoezi la kuwanyang'anya wanajeshi silaha, mchakato unaofanywa
na vikosi vya kijeshi kutoka Ufaransa, vinavyofanya operesheni maalum mjini Bangui,
ambako hivi karibuni watu mia nne walipoteza maisha yao kutokana na mapigano.