2013-12-11 08:29:35

Mlango wa Bwana daima ni wazi na kutupatia tumaini.


Hatupaswi kuhofia ukombozi wa Bwana , badala yake , ni kujiweka tayari kwa ajili ya ujio wake. Ni kuufungua mlango wa moyo na kumpokea kwa matumaini. Papa alieleza katika homilia yake wakati wa Ibada ya Misa, mapema asubuhi Jumanne, katika Kanisa dogo la Mtaktifu Marta hapa Vatican.

Papa alitafakari maneno ya somo la kwanza, kutoka Kitabu cha Nabii Isaya, ambamo Nabii Isaya anasema, "farijikeni enyi watu wangu, Bwana, yu karibu na watu wake, kuwatuliza ,na kuwapa amani". Papa ameeleza kazi hii ya kufariji, ina uwezo wa kubadili yote. Bwana, kweli ana uwezo wa kuviumba vyote upya .

Bwana hufanya vyote kuwa vipya . Na kanisa Kamwe halichoki kutangaza habari hii ya uwezo wake wenye nguvu ya kufanya vitu vyote upya ,na huvifanya katika maajabu yake. Na kwa namna hiyo , huwatembelea watu wake, akiwafanya kuwa viumbe wapya, kwa uwezo wake Mkuu. Papa alieleza kwa kurejea pia maneno ya mwisho ya Yusuf kwa ndugu zake , kwamba , Bwana atawatembelea. Na wakati Bwana atakapo watembelea, wachukue pia mifupa yake pamoja nao. Bwana kutembelea watu wake, lilikuwa ni tumaini la Israeli. Na aliwatembelea na kuwafariji.

Akiendelea kufafanua maana kutembelea na kufariji , alisema, Bwana hufanya hivyo mara nyingi tu, hata kwetu pia, katika ulimwengu huu wetu. Papa alisisitiza mambo mawili, kwamba, Wakati Bwana atakapokuja atatupa tumaini ,ambalo ni lina uwezo wa kweli katika maisha yote ya Kikristu. Hii ni neema,na ni zawadi.

Na akaonya kwamba, pale Mkristu anaposahau tumaini hili, au mbaya zaidi kupoteza matumaini, maisha yake pia hupoteza maana. Lakini Bwana hachoki kuwapokea wanao mrejea , na huwafariji na kuwapa tumaini jipya. Na hufanya hivyo kwa upole mkuu na huwa karibu na kila mmoja wetu , kwa sabab u yeye huwafariji wake wake na humfariji kila mmoja wetu. Yeye ni Mchungaji mwema mwenye kulichunga kundi lake la kondoo, kw amkono wake huwakusanya wanakondoo na kuwapeleka kaika malisho yake mazuri na kuwahudumia kwa wema wote..

Papa alieleza na kumalizia kwa kutazama jinsi Yesu alivyoishi na wafuasi wake , Maria Magdalene na wale wanafunzi wa Emmaus . Pia kwa Tomas aliyemwambia weka kidole chako hapa. Hivyo ndivyo Bwana alivyowafariji na kuwapa tumaini wanafunzi wake. Papa alisali ili Bwana atupatie sisi sote neema ya kutoogopa kufarijiwa na Bwana , bali kuwa tayari kufungua mlango wa moyo na kumwomba neema hii ya matumaini na kuwezeshwa kuusikia wema wa Mungu Baba.







All the contents on this site are copyrighted ©.