Kardinali Peter Turkson , kumwakilisha Papa katika mazishi ya Mandela
Baba Mtakatifu Francisko , amemteua Kardinali Peter Turkson, Rais wa Baraza la Kipapa
kwa ajili ya Haki na Amani , kuwa mwakilishi wake maalum, wakati wa Maziko ya Rais
Mstaafu wa Afrika Kusini Nelson Mandela. Nelson Mandela alifariki Alhamisi ya
wiki iliyopita akiwa na umri wa miaka 95, kwa maradhi ya mapafu. Mwana huyo maarufu
wa Afrika. Jumanne tarehe 10 Desemba 2013, watu watapata nafasi ya kutoa heshima zao
za mwisho na maziko ni hapo jumapili tarehe 15 Desemba 2013.