Baba Mtakatifu Francisko ametuma salam za rambirambi kwa Rais Jacob Zuma wa Afrika
ya kusini na wananchi wa Afrika ya Kusini kwa ujumla wao kutokana na kifo cha Mzee
Nelson Mandela. Anaiombea roho ya Mzee Mandela iweze kupata huruma ya Mungu pamoja
na kuendelea kuwaimarisha wote walioguswa na msiba huu mzito!
Baba Mtakatifu
Francisko anasema, Mzee Nelson Mandela alisimama kidete kulinda na kutetea utu na
heshima ya raia wake; akajenga na kuimarisha umoja wa wananchi wa Afrika ya Kusini
pasi na vita, wakitembea katika njia ya upatanisho na ukweli.
Ni matumaini
ya Baba Mtakatifu kwamba, mchango wa Mzee Mandela utakuwa ni changamoto kwa wananchi
wa Afrika ya Kusini kusimama kidete kulinda haki na mafao ya wengi; wanasiasa wakiwa
mstari wa mbele. Baba Mtakatifu anawapatia wananchi wote wa Afrika ya Kusini baraka
zake za kitume, wakati huu wa maombolezo ya kitaifa!