2013-12-06 14:13:24

Nelson Madiba Mandela mfano wa kiongozi bora- Obama


Viongozi mbalimbali wa dunia wanapeleka salaam zao za rambirambi kwa familia ya Nelson Mandela na raia wote wa Afrika Kusini kufuatia kifo cha Nelson Madiba Mandela. Rais Barack Obama, wa Marekani katika salam zake za rambirambi, ameikumbuka historia ya Nelson Madiba Mandela na kueleza kuwa yeye Obama ni kati ya mamilioni ya watu waliovutiwa sana na ushujaa wa Nelson Madiba.

Obama ametaja machache yaliyomvuitia toka kwa Madiba kuwa ni pamoja na maneno aliyo yatoa wakati wa kesi yake mwaka 1964, ambako akiwa kizimbani alisema, ' Nimepigana kwa bidii dhidi ya udhalimu wa utawala wa wazungu wachache, na pia dhidi ya utawala wa weusi wachache.

'Mimi ninapendelea jamii yenye demokrasia, jamii huru, ambamo watu wote wanaishi kwa amani na fursa sawa. Ni mawazo ninayotumiani kuyaishi na kuyafanikisha , hata kama italazimu kifo kwa ajili hiyo. Rais Obama anasema, kweli Nelson Mandela aliishi kwa lengo hilo , na alilifanikisha na leo hii ametutoka kwa amani. Ni lengo linalotakiwa kufanikishwa na kila binadamu.

Na kwamba, dunia imempoteza moja wa watu mashuhuri, jasiri, mwama na diliafu, anayefaa kuigwa na binadamu wote, katika maisha ya hapa duniani. Yeye daima atakuwa mfano wa maisha bora. Na kupitia heshima na unyenyekevu na mapenzi yake thabiti katika kujitolea sadaka kwa ajili ya uhuru wake mwenyewe na uhuru wa watu wengine, Madiba kwa kushirikiana na wengine aliibadili Afrika Kusini.

Rais Barack Obama ameomba , safari ya Madiba tangu kuwa mfungwa gerezani hadi Urais, na iangaze na kutoa uvuvio kwa kila binadamu katika kubadili ubaya na kuwa wema na katika kudumisha ahadi ya kusamehe, amani na mapatano, si nchini mwake tu lakini katika mataifa yote na hata katika maisha yetu binafsi.Huo ndiyo urithi mkuu ulioachwa na Madiba kwa dunia yote.








All the contents on this site are copyrighted ©.