Askofu msaidizi Monfort Stima ateuliwa kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Mangochi,
Malawi
Baba Mtakatifu Francisko, tarehe 6 Desemba 2013 amekubali ombi la kung'atuka kutoka
madarakani lililotolewa na Askofu Alessandro Pagani, S.M.M. kadiri ya sheria za Kanisa
namba 401ยง 1. Baba Mtakatifu ameteua Askofu msaidizi Monfort Stima wa Jimbo kuu la
Blantyre, kuwa Askofu mpya wa Jimbo la Mangochi, nchini Malawi.