2013-12-04 15:22:15

Viongozi wapya wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Jakaya Mrisho Kikwete amewapandisha vyeo Maafisa Wakuu wanne wa Jeshi la Polisi Tanzania. Aidha, Rais Kikwete amefanya uteuzi wa nafasi za madaraka katika Jeshi hilo kufuatia mabadiliko ya muundo wa Jeshi la Polisi Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Ikulu, Dar Es Salaam, Jumanne, Desemba 3, 2013 na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Dr. Florens Turuka waliopandishwa vyeo kuwa Kamishna wa Polisi (CP) na ambao wote walikuwa ni Naibu Kamishna wa Polisi ni DCP Ernest Mangu, DCP Thobias Andengenye, DCP Abdulrahaman Kaniki na DCP Hamdan Omari Makame.

Rais pia amempandisha cheo SACP Athuman Diwani kuwa Naibu Kamishna wa Polisi. Walioteuliwa katika nafasi za madaraka katika Jeshi la Polisi ni CP Clodwing Mtweve ambaye anakuwa Kamishna wa Fedha na Utaratibu wa Ugavi na Usafirishaji wa Watu na Vitu (Logistics), CP Paul Chagonja ambaye anakuwa Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, CP Isaya Mungulu ambaye anakuwa Mkurugenzi wa Uchunguzi wa Makosa ya jinai (DCI), CP Mussa Ali Mussa ambaye ameteuliwa kuwa Kamishna wa Polisi Jamii.

Wengine ni CP Hamdan Omari Makame ambaye anakuwa Kamishana wa Polisi, Zanzibar; CP Ernest Mangu ambaye anakuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Jinai, CP Thobias Andengenye ambaye anakuwa Kamishna wa Utawala na Utumishi, CP Abdulrahman Kaniki ambaye anakuwa Kamishna wa Uchunguzi wa Ushahidi wa Jinai na CP Abdulrahman Diwani ambaye anakuwa Naibu Mkurugenzi wa DCI.








All the contents on this site are copyrighted ©.