2013-11-30 08:37:13

Mkuu wa Jumuiya ya Taizè akutana na Papa Francisko


Brother Alois, Mkuu wa Jumuya ya Taize , Alhamis, alipokelewa Vatican na kukuana na Papa Francisko akifuata nyayo za mtagulizi wake Brother Roger mwanzilishi wa Jumuiya ya Taize, ambaye kila mwaka alifika Vatican kukutana na Papa.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari, ziara yake ya Brother Alyosius kwa Papa Francisko aliifanya katika mazingira ya faragha, kama ilivyokuwa miaka ya nuuma alipokutana na Papa Benedikto XV1. Brother Roger,wakati wake alikutana na Papa Yohane wa XXIII, Papa Paul VI na Papa Yohane Paul II.

Alhamis iliyopita Brother Alosius katika maongezi yake na Papa Francisko, alieleza jinsi wanavyowapokea vijana katika jumuiya ya Taize na hija ya kiroho wanaoifanya kama hatua ya kuhamasisha vijana kiroho kutoka mabara yote. Na Papa alizungumzia tukio hili la kiekumene la Taizé kwamba ubatizo, ni daraja linalo waungnaisha wote na kuwapa nguvu za kutembea pamoja katika njia hii ya kiekumene.







All the contents on this site are copyrighted ©.