Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anasema
kwamba, kwa watu wengi kusamehe ni jambo gumu sana. Anawaalika waamini kumwomba Yesu
Kristo ili aweze kuwasaidia kuwa na moyo wa huruma, tayari kusamehe na kusahau kama
njia ya kuonjeshana upendo na huruma ya Mungu katika hija ya maisha ya hapa duniani.