2013-11-28 10:58:06

Mkutano wa kimataifa dhidi ya adhabu ya kifo duniani


Jumuiya ya Mtakatifu Egidio yenye makao makuu yake mjini Roma, tangu mwaka 2002 imekuwa ikiendesha kampeni dhidi ya adhabu ya kifo duniani inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 30 Novemba. Hii ni tarehe ambayo Umoja wa Ulaya ulifuta adhabu ya kifo mjini Toscana, kunako tarehe 30 Novemba 1786.

Tangu Mwaka 2002 Majiji na Miji ipatayo 80 inajiunga katika tukio hili linaloonesha umuhimu kwa Jumuiya ya Kimataifa kusimama kidete kulinda na kutetea zawadi ya maisha. Mwaka huu, zaidi ya miji 1600 itashiriki katika kampeni dhidi ya adhabu ya kifo na kati ya miji hii, kuna miji mikuu 70 kutoka sehemu mbali mbali za dunia. Matukio mbali mbali yanatarajiwa kufanyika kwenye miji hii kama sehemu ya maadhimisho ya kampeni dhidi ya adhabu ya kifo duniani.

Ijumaa tarehe 29 Novemba 2013 kunafanyika mkutano wa kimataifa kuhusu kupinga adhabu ya kifo unaohudhuria na wajumbe kutoka sehemu mbali mbali za dunia, lakini Bara la Afrika kuna wawakilishi kutoka Tanzania, Msumbiji, Senegal, Burkina faso, Pwani ya Pembe, Guinea Bissau, Guinea Conakry, Namibia, Niger, Togo, Ethiopia, Gabon, Rwanda na Morocco.

Hata leo hii bado kuna nchi ambazo zinetekeleza adhabu ya kifo, ingawa kunako tarehe 20 Desemba 2012 Baraza kuu la Umoja wa Mataifa lilipisha kwa kura nyingi marathoni dhidi ya adhabu ya kifo. Baadhi ya nchi hizi ni Gambia, Japn, India, Pakistan na Iraq na China.







All the contents on this site are copyrighted ©.