2013-11-28 15:42:36

Imani si jambo binafsi, bali ni mwaliko kwa wote- Papa Francisko asema...


Imani si jambo binafsi, lakini ni mwaliko ulio wazi kwa watu wote, kumwabudu Mungu mpaka mwisho wa maisha licha ya hatari ya kupambana na changamoto za maisha ya mateso na kukatishwa tamaa na uovu.

Papa ameeleza na kuonya kwamba, kuna nguvu ya kidunia, yenye kutaka kuifanya dini kuwa kama ni suala binafsi. Lakini Mungu, ambaye ameshinda dunia , anaendelea kuipenda na kuutangaza uongofu wa kutembea katika njia ya imani na Yesu Kristu katika ukamilifu na uaminifu wake,Papa alionya wakati wa Ibada ya Misa, Alhamsi hii mapema asubuhi, katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta ndani ya Vatican.
Papa amesema Wakristo wanaoteswa leo hii , ni ishara ya mtihani, juu ya ushindi wa Yesu dhidi ya shutuma na madhulumu aliyopambana nayo.
Homilia ya Papa ililenga katika mapambano ya mwisho, kati ya Mungu na maovu , kama masomo ya liturujia katika kipindi cha kufunga mwaka yanavyo tahadharisha, kuwa macho na mitego yote ya dhambi, ambayo Papa ameiita kuwa majaribu ya dunia. .

Majaribu ya kukabiliwa na mvuto wa kumuasi Mungu kutoka kwa wale ambao wanaonekana kw amaovu wanayoyafanya , kama vile wamemshinda Mungu, na kuonekana kuw ana maisha bora zaidi katika jamii, wingi wa vitu na mali, zaidi ya wale wenye kumuamini Mungu. Lakini Papa anaeleza kwa Muumini vitu na mali si kitu kwake, kwa kuwa havimpi tumaini la kudumu na ushindi dhdi ya mauti, ushindi unaoelezwa katika rejea wazi ya ushindi na tumaini lililoletwa na Yesu, aliye yashinda majaribu jangwani na kisha katika maisha yake ya umma,ambamo alivumilia yote, matusi na Kashfa na kutoheshimiwa hadi kifo cha aibu msalabani. Kifo kilichoonekana kama Mfalme wa Ulimwengu ameshindwa vita, lakini akadhihirisha kuwa ni Mkuu wa amani kwa utukufu wa ufufuko wake, baada ya kulala kaburini kwa siku tatu.

Papa Francisko amesema, hii inaonyesha hatua za maisha ya Kristu, katika kufanikisha mageuzi duniani. Ni kuushupalia ukweli wa imani na kuvumilia yote katika hali ngumu za manyanyaso na mateso. Papa alilenga moja kwa moja kwa katika somo la Injili, ambamo Yesu, anatabiri kuharibiwa kwa mji wa Jerusalem na kunajisiwa kwa imani .
Papa Francis, amewatia moyo Wakristu kwamba, katika majaribu ya mateso na madhulumu , hakuna sababu za kuwa na hofu au kuogopa kuuishi Ukristu kwa uaminifu, kw akuwa kama ilivyokuwa wakati wa Yesu mateso namadholumu hayo yanamuimarisha muumini katikakutembea karibu na Yesu kuielekea Jerusalem mpya ya milele. Yesu anawataka waamini wake kuwa aminifu na kuvumilia, kama ilivyokuwa kwa Daniel , ambaye alikuwa mwaminifu kwa Mungu wake na kuabudu Mungu mpaka mwisho kwa kuwa, aliyasadiki ahadi ya Mungu " hakuna unywele wa kicha cha muumini utakao anguka bure"Hii ni ahadi ya Bwana, na tuombe neema na majaliwa ya kusadiki hili, Papa Francisko ameomba.








All the contents on this site are copyrighted ©.