Askofu Balthason Ramaroson ateuliwa kuwa Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Antsiranana,
Madagascar
Baba Mtakatifu Francisko, tarehe 27 Novemba 2013 amekubali ombi la Askofu mkuu Michel
Melo kung'atuka kutoka madarakani kadiri ya sheria za Kanisa namba 401ยง 1 na badala
yake Baba Mtakatifu amemteua Askofu Benjamin Marc Balthason Ramaroson kuwa Askofu
mkuu wa Jimbo kuu la Antsiranana, nchini Madagascar.
Kabla ya uteuzi huu, Askofu
mkuu mteule Balthason Ramaroson alikuwa ni Askofu wa Jimbo Katoliki Farafangana.