2013-11-27 15:42:13

Maisha ni maandalizi ya uzima wa milele! Papa Francisko asema..


Jumatano hii , Baba Mtakatifu akitoa mafundisho yake kwa mahujaji na wageni waliokusanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, wapatao 50,000, kwanza aliwashukuru na kuwapongeza kwa moyo wao wa kupenda kusikiliza mafundisho ya Papa licha ya hali ya baridi iliyokuwepo uwanjani hapo.

Katika hotuba yake, Papa alieleza kwamba leo anakamilisha katekesi zake juu ya sala ya imani, sala ya Nasadiki, ambayo amekuwa akiizungumzia katika kipindi cha maadhimisho ya mwaka wa imani, ulio kamilika Jumapili iliyopita.. Leo Papa ametafakari juu ya Ufufuko wa Mwili, kama iiivyo katika mafundisho ya Kateksimo ya Kanisa Katoliki.......

Alianza kusema, ndugu zangu wapendwa, napenda kuikamilisha katekesi hii ya Imani kwa kutafakari juu ya ufufuo wa mwili. Imani ya Kikristo hutumulikia katika fumbo la kifo na matumaini katika ufufuko. Kifo ni changamoto kwetu sote. Mbali na imani kwa Mungu, na muono wa maisha kama ni hali katika uwepo wa dunia , kifo kinaonekana kuwa ni janga la kutisha , na kutufanya tupoteza maana yake, kikileta hofu kali ya kutaka kujiweka mbali nacho. Lakini kumbe binadamu aliumbwa na jambo moja kuu, ambalo humpatia hamu ya kuwa katika uwepo usio na mipaka, umilele.

Papa aliendelea kufundisha kwamba, Ufufuko wa Kristo si tu hutuonyesha uwepo wa maisha zaidi baada ya kifo, lakini pia hutuonyesha maana ya kweli ya kifo, kwamba, tunakufa kwa ajili ya kuishi upya: iwapo maisha yetu haya ya nyama na damu yatakuwa katika muungano na upendo na Mungu. Katika kuishi na Mungu, tunapata uwezo wa kuachana na maisha haya katika hali ya utulivu na ujasiri wa kujiweka katika mikono ya Mungu wakati wa kifo chetu.

Papa alikumbusha , Bwana wetu mara nyingi anatuambia kuwa waangalifu namanabii wa uongo, akijua kwamba , maisha yetu katika dunia hii , ni kwa ajili ya maandalizi ya maisha yajayo. Kama tunabaki karibu naye, hasa kwa njia ya kuwapenda maskini na kuwa na mshikamano na wahitaji, hakuna haja ya kukiogopa kifo, bali ni kukipokea kifo kwa furaha wakati mlango wa mbinguni upofunguliwa kwa ajili ya kuingia katika furaha ya uzima wa milele.







All the contents on this site are copyrighted ©.