2013-11-26 15:56:16

Papa Francisko atoa "Encyclical" yake ya kwanza: “Evangelii Gaudium”


Askofu Mkuu Claudio Celli , Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Mawasiliano Jamii, Jumanne 26 Novemba 2013, amewasilisha kwa wanahabari, waraka wa kitume wa kwanza wa Papa Francisko juu ya utangazaji wa Injili katika Dunia ya leo.
Askofu Mkuu Celli, akiuzungumzia waraka huu, alitaja mambo mawili kwanza mtindo na lugha iliyotumika akisema kwamba, mna tabia ya kina yenye kutoa msukumo wa kichungaji. Kama Papa Francisko yeye mwenyewe anavyosema, kwamba, anatamani kuufikisha ujumbe huu kwa Wakristu wote, kuwakaribisha katika hatua mpya ya uinjilishaji.
Askofu Mkuu Celli anasema , hivyo katika kuusoma waraka huu, mnatoa changamoto kwa wachungaji, kufanya mazungmzano na tafakari na Walei. Papa amehimiza utumiaji wa lugha nyepesi na unyenyekevu kama inavyojionyesha katika hotuba na homilia zake katika kipindi hiki cha miezi michache ya utawala wake.
Askofu Mkuu Claudio ametaja kipengere kingine kilicho sisitizwa na Papa katika waraka huu kuwa ni jukumu la mawasiliano katika hatua hii mpya ya uinjilishaji. Papa anataka kuonyesha, njia ambamo Kanisa linatakiwa kutembea katika miaka ijayo.
Askofu Mkuu Celli anasema, ni dhahiri , zaidi ya yote, Papa Francisko anafahamu kile kinachoendelea katika ulimwengu wa leo , hasa katika uwanja wa afya, elimu na mawasiliano. Kwa ufahamu na utambuzi alionao katika maendeleo na mafanikio ya mtu kwa wakati huu, hasa katika mambo yanayohusiana na ubunifu dhahiri teknolojia , anasema, tuko katika enzi ya ubunufu, maarifa na mawasiliano, chanzo cha aina mpya ya nguvu.
Katika mtazamo huo, Papa ametahadharisha hasa katika utoaji wa homilia akisema, inafaa kujua tatizo, si tu kujua nini cha kusema lakini hasa kwa namna gani kutakuwa na mwendelezo wake. Kwa ajili hii Papa Francisko, anasisitiza mahubiri mepesi yanayoweza kutoa picha nzuri kwa wanaosikiliza. Mahubiri mazuri nyeye kutoa wazo , hisia, picha.
Pia Papa anakumbusha daima suala la lugha , akikumbusha umuhimu wa unyenyekevu katika lugha inayotumika. Ni lazima kuwa na lugha nyepesi ya kueleweka na si kuzunguka zunguka.
Askofu Mkuuu Claudio Celli, amekamilisha pamoja na maelezo mengine alikamilisha hotuba yake kwa kutoa mtazamo zaidi wa Papa Francisko , katika mawasiliano kwenye shughuli za Kanisa , akisema ni lazima, mawasiliano yaonyesha maana ya shughuli za Kanisa. Na hivyo wahusika wanapaswa kuwa na ujasiri wa kupata ishara mpya , alama mpya, nyama mpya kwa ajili ya maambukizi ya neno, aina mbalimbali za uzuri kuwa wazi wenyewe katika nyanja mbalimbali za kitamaduni. Na hii ni changamoto, inayotolewa na Papa Francisko, kwa kila muumini wa kanisa. .









All the contents on this site are copyrighted ©.