2013-11-26 11:25:55

Mkutano wa Syria kimataifa sasa kufanyika tarehe 22 Januari 2014


Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon ametangaza kwamba, mkutano wa kimataifa unaotarajiwa kuzungumzia kuhusu hali ya amani na usalama nchini Syria, utafanyika tarehe 22 Januari 2014 mjini Geneva. Mkutano huu ni daraja la kipindi cha mpito nchini Syria ili kujenga na kuimarisha uhuru na utu wa wananchi wa Syria ambao kwa miezi ya hivi karibuni wameendelea kukumbana na majanga ya maisha.

Ulinzi na usalama ni kati ya vipaumbele vinavyotolewa na Umoja wa Mataifa kwa wakati huu. Wadau wakuu katika mkutano wa Geneva ambao ulikuwa unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi Novemba, 2013 walikuwa ni Marekani na Russia, umefutwa baada ya pande zinazohusika kushindwa kuafikiana katika masuala nyeti! Iran na Saud Arabia zinatarajiwa kushiriki katika mkutano huu kadiri ya taarifa za kidiplomasia.







All the contents on this site are copyrighted ©.