2013-11-26 11:55:37

Kiasi cha dolla millioni 1 kugharimia miradi ya maendeleo kwa Kanisa Barani Afrika


Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani katika mkutano wao wa mwaka uliohitimishwa hivi karibuni mjini Bartimore, umepitisha kiasi cha dolla za kimarekani 948, 195 zitakazogharimia miradi 38 inayolenga: majiundo ya shughuli za kichungaji; haki na amani: uongozi na gharama za uendeshaji. DRC ni kati ya nchi ambazo zitafaidika zaidi na msaada huu kutokana na kuathirika kwa vita ambayo imekuwa ni chanzo cha majanga mengi nchini humo.

Majimbo mengi Barani Afrika yameanza kuonesha cheche za kujitegemea kumbe, msaada unaotolewa ni kwa ajili ya maboresho ya miundo mbinu na majiundo endelevu anasema Kardinali Theodore McCarrick, Mwenyekiti wa Tume Ndogo ya Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani kwa ajili ya Kanisa Barani Afrika.

Burkina Faso itasaidiwa katika maboresho ya njia za mtandao, madarasa na majiundo makini kwa ajili ya walimu, ambao wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu. Shule ni mahali ambapo wanafunzi wamebahatika kurithishwa imani, maadili na utu wema. Msaada huu unapania kuliwezesha Kanisa Barani Afrika kujikita zaidi na zaidi katika elimu, kama njia ya kuwaonjesha wengine ile Furaha ya Injili.







All the contents on this site are copyrighted ©.