MDM yakitoa jasho chama cha Frelimo nchini Msumbiji!
Tangu baada ya Msumbiji kujinyakulia uhuru wake kutoka kwa Mreno, Chama cha Frelimo
kimekuwa kikishinda kwa kishindo, lakini uchaguzi wa serikali za mitaa uliohitimishwa
hivi karibuni nchini humo unaonesha kwamba, kuna mabadiliko makubwa miongoni mwa wapiga
kura kwa watu kuonesha upendeleo kwa Chama cha Mageuzi Msumbiji, MDM.
Hiki
ni chama ambacho ni cha tatu kwa ukubwa baada ya Renamo ambacho kilisusia uchaguzi
huo na kutishia kurudi tena msituni kuendesha mapambano ya silaha. Wachunguzi wa masuala
ya kisiasa nchini Msumbiji wanasema kwamba, Frelimo itashinda kwa asilimia kubwa,
lakini kwa sasa inaanza kupata wapinzani wanaoendelea kujiimarisha katika uwanja wa
demokrasia hasa katika miji mikubwa nchini Msumbiji.