Waamini wanaoteseka kutokana na imani kwa Kristo na Kanisa lake, wakumbukwa na Papa!
Mara baada ya Maadhimisho ya Sherehe ya Yesu Kristo Mfalme wa Ulimwengu sanjari na
kufunga Mwaka wa Imani, kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, Baba Mtakatifu
aliwatakia kheri na baraka wote waliomiminika kwa wingi katika Ibada ya Misa Takatifu
kutoka ndani na nje ya Italia.
Amewasalimia kwa namna ya pekee, washiriki
wa kongamano la kitaifa la Huruma ya Mungu; Jumuiya ya waamini kutoka Ucrain, wanapofanya
kumbu kumbu ya miaka 80 tangu ilipotokea njaa kubwa inayojulikana kama "Holodomor"
iliyosababisha watu zaidi ya millioni moja kupoteza maisha.
Baba Mtakatifu
amewakumbuka Wamissionari kutoka sehemu mbali mbali za dunia waliojitosa kimasomaso
kutangaza Injili ya Kristo hadi miisho ya dunia. Kati yao amemkumbuka Mwenyeheri Junìpero
Serra, Mmissionari kutoka katika Shirika la Wafranciskani anayekumbukwa kwa kutimiza
miaka mia tatu tangu alipozaliwa. Katika sala ya Malaika wa Bwana, Baba Mtakatifu
amewakumbuka waamini wote wanaoteseka na kudhuliwa kutokana na imani na uaminifu wao
kwa Kristo na Kanisa lake.