Askofu Thomas Msusa ateuliwa kuwa Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Blantyre, Malawi
Baba Mtakatifu Francisko amemteuwa Askofu Thomas Msusa kuwa Askofu mkuu wa Jimbo kuu
la Blantyre, Malawi. Kabla ya uteuzi huu, Askofu Msusa alikuwa ni Askofu wa Jimbo
Katoliki la Zomba.
Askofu mkuu mteule alizaliwa kunako tarehe 2 Februari 1962
Wilyani Mangochi. Baada ya masomo na mjiundo yake ya Kipadre, akapewa daraja takatifu
la Upadre hapo tarehe 3 Agosti 1996. Tarehe 16 Januari 2004 akateuliwa kuwa Askofu
wa Jimbo Katoliki Zomba na kuwekwa wakfu kuwa Askofu hapo tarehe 17 Aprili 2004.