Wasaidieni wahamiaji kutambua: utamaduni, mila na desturi zao, ili kumwilisha tunu
za Kiinjili mahali wanapoishi!
Historia ya Poland imefumbata pamoja na mambo mengine matukio yaliyopelekea wananchi
wengi wa Poland kuikimbia nchi yao. Hali hii iliwakumbuka hata waamini wa Kanisa Katoliki,
hali ambayo ililihamasisha Kanisa kuibua mbinu mkakati kwa ajili ya kuwahudumia wahamiaji
na wakimbizi waliokuwa wanaishi ugenini.
Huu ukawa ni mwanzo wa Mapadre wa
kiroho wanaojitoa kwa ajili ya wakimbizi pamoja na wahamiaji katika hija ya maisha
yao ya kila siku. Mapadre wanaowahudumia wahamiaji na wakimbizi wanatekeleza dhamana
na utume wao kama Mashemasi wa huduma ya umoja na mshikamano. Wanapaswa kuhakikisha
kwamba, wanalinda na kudumisha utambulisho wa mahali wanapotoka wahamiaji na wakimbizi
kwa kuzingatia: tamaduni, mila, desturi na ibada zao.
Wana wajibu wa kuwasaidia
kujishikamanisha na Jamii inayowazunguka pamoja na Kanisa mahalia. Kwa njia hii, wahamiaji
na wageni wanaweza pia kumwilisha ndani mwao ari na moyo wa kimissionari tayari kujitosa
kimasomaso kwa ajili ya kutangaza Injili ya Kristo kwa njia ya ushuhuda wa maisha
yao hata wanapokuwa ugenini!
Ni maneno yaliyotolewa na Kardinali Antonio Maria
VegliĆ², Rais wa Baraza la Kipapa la shughuli za kichungaji kwa ajili ya wahamiaji
na watu wasiokuwa na makazi maalum wakati wa hija yao ya kichungaji mjini Roma, kuanzia
tarehe 19 hadi tarehe 21 Novemba 2013.