2013-11-19 09:27:25

Sheria mpya kuhusu fedha yapitishwa na Papa Francisko


Baba Mtakatifu Francisko kunako tarehe 14 Novemba 2013 alitia sahihi barua ya kitume iliyopitisha Katiba na Sheria za Mamlaka ya Intelijensia ya Fedha, (F.I.A.), ambazo zitaanza kutumika tarehe 21 Novemba 2013. Ni sheria ambazo zinakazia pamoja na mambo mengine kuhusu: ukweli na uwazi, Usimamizi na intelijensia katika masuala ya fedha.

Baba Mtakatifu ameimarisha sheria hizi kwa ajili ya mji wa Vatican ili kuhakikisha kwamba, shughuli za fedha zinazingatia sheria, kanuni na maadili kama inavyotakiwa. Baba Mtakatifu Francisko amefanya maboresho kwenye sheria zilizokuwa zimekwisha idhinishwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, hapo tarehe 30 Desemba 2010 kwa kutaka wadau kutekeleza dhamana hii nyeti kwa kuzingatia kanuni, maadili, weledi na taaluma yao.

Sheria mpya inafafanua dhamana na majukumu ya Rais, Bodi ya Wakurugenzi na Uongozi ili kuhakikisha kwamba, Mamlaka ya Intelijensia inafanya kazi zake barabara.







All the contents on this site are copyrighted ©.