Waziri mkuu wa Bahamas akutana na Papa Francisko mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 18 Novemba 2013 amekutana na kuzungumza
na Waziri mkuu wa Bahamas Perry Gladstone Christie na ujumbe wake ambao pia umekutana
na viongozi waandamizi kutoka Vatican chini ya Askofu mkuu Pietro Parolin, Katibu
mkuu wa Vatican.
Viongozi hawa wawili wamejadili pamoja na mambo mengine kuhusu
uhamiaji na mchango wa Kanisa katika maendeleo ya wananchi wa Bahamas, hususan katika
sekta ya elimu na kwamba, wameonesha utashi wa kutaka kuimarisha ushirikiano wao katika
medani mbali mbali za maisha.