2013-11-16 14:59:52

Simameni kidete kupinga utamaduni wa kifo, kumbatieni matumaini ya zawadi ya maisha!


Waamini, watu wenye mapenzi mema, vyama vya kitume na kiraia, Jumapili tarehe 17 Novemba 2013 vinafanya maandamano makubwa nchini Hispania kupinga tabia ya baadhi ya viongozi kukumbatia sera na utamaduni wa kifo! Wanapenda kutoa mwaliko wa kusitisha sera za utoaji mimba na kuanza mchakato wa matumaini yanayokumbatia zawadi ya uhai kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Haya ni maandamano ya nne kufanyika nchini Hispania katika harakati za kupinga utamaduni wa kifo.

Maandamano haya ni kielelezo cha sauti ya Familia ya Mungu nchini Hispania kuiomba Serikali yao kusimama kidete kulinda na kutetea zawadi ya uhai, kama walivyoahidi wakati wa kampeni ya kutaka kuingia madarakani, lakini inaonekana kwamba, mara tu baada ya kuingia madarakani, wamesahau ahadi yao na kuanza kukumbatia utamaduni wa kifo, kwa kupitisha sera na sheria zinazohalalisha utoaji mimba nchini Hispania. Waamini na watu wenye mapenzi mema wanasema, utoaji mimba uwe zero! watu wajenge utamaduni wa kuenzi zawadi ya uhai bila masharti!







All the contents on this site are copyrighted ©.