2013-11-14 16:15:14

Rais Giorgio Napolitano ampokea Papa katika jengo la Ikulu ya Italia.


Rais Giorgio Napolitano,Alhamis hii 14 Novemba 2013, majira ya saa nne alimpokea Papa Francisko, aliyemtembea akiwa katika makazi ya Ikulu ya Italia inayojulikana kwa jina la Quirinale, yaliyoko katikati ya jiji la Roma.

Rais Napolitano katika hotuba yake ya mapokezi, hakuficha furaha yake ya kutembelewa na Papa akisema anaona kama ni upendeleo fulani, na pia ugeni wake ni ushuhuda wa mwendelezo wa historia ya muda mrefu katika mahusiano mazuri kati ya Rais wa Italia na Mkuu wa Kanisa Katoliki la Ulimwengu, yaani Papa .

Na kwamba uwepo wa uwakilishi muhimu wa viongozi wa Jamhuri ya Italia na taasisi zingine za serikali na mashirika ya kijamii, ulimwengu wa utamaduni na dunia Katoliki , ni ishara wazi kwamba, inawezekana pia kuwa na mshikamano wa karibu zaidi katika utendaji kwa ajili ya kusaidia watu maskini na wanaoteseka kwa saba bu mbalimbali hasa majanga asilia, na mabavu mengine yaliyo nje ya uwezo wao.

Rais Napolitano alitoa shukurani zake kwa Papa Francisko akisema, watu wote - waumini na wasio waumini, wanaguswa na hotuba za Papa ambazo anazitoa kwa maneno mepesi lakini yenye nguvu. Na wengi wameweza kupata mwamko wa kuona ukosefu au udhaifu katika ushupavu, wa kupambana na changamoto za dunia, ambazo viongozi wengi,wanapenda kujiweka mbali nazo na kuona kama si jukumu hilo, hasa kutokana na mashaka na wasiwasi wa hali nchi zao kwa baadaye, iwe kisiasa au kitamaduni na hata kiimani.

Lakini kwa hotuba zake Papa Francisko na watangulizi wake, pamoja na kusoma upya yaliyomo katika waraka wa Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, wameweza kuangaziwa upya na roho wa Injili kwamba uwajibikaji wa kanisa katika masuala ya Kijamii ni kutetea tunu msingi za ubinadamu kwa watu wote.

Na hivyo, watu wengi sasa wanaona fukuto la matarajio mpya, katika mazungumzano na watu mbalimbali , hasa zaidi na wapinzani, kwamba , ni muhimu kuwa na mahusiano ya karibu na kufanyakazi pamoja kwa ajili ya udumishaji yaliyo mema kwa watu wote, kama ambavyo,Papa Francisko, amekuwa ukisistiza katika hotuba zake, kwamba ni lazima kujitahidi kujenga ushirikiano wa karibu , kwa ajili ya kupambana na changamoto za kipekee za kisasa, na hasa katika ujenzi wa mustakabali, kupitia uhamasishaji wa dhamiri na nishati na zaidi ya yote maadili.... Na kwamba Papa Francisko,amekuwa ni mfano mzuri wa kuigwa na viongozi katika utimizaji wa ahadi wanazo toa.







All the contents on this site are copyrighted ©.