2013-11-14 12:29:42

Onesheni mshikamano wa upendo kwa wananchi wa Ufilippini kwa kuchangia kwa hali na mali!


Baraza la Maaskofu Katoliki Italia limeupokea wito na mwaliko wa Baba Mtakatifu Francisko anayewataka waamini na watu wote wenye mapenzi mema kujiunga katika mapambano yanayopania kuokoa maisha ya wananchi wa Ufilippini waliokumbwa na majanga hivi karibuni kama njia ya kuonesha mshikamano wa upendo kwa hali na mali.

Baraza la Maaskofu Katoliki Italia linatangaza kwamba, tarehe Mosi, Desemba 2013 itakuwa ni siku maalum ya mshikamano na ananchi wa Ufilippini. Waamini na watu wenye mapenzi mema wanaalikwa kuchangia kwa hali na mali katika jitihada za kuokoa maisha ya watu wengi wanaohitaji msaada wa dharura kwa sasa. Hadi sasa Shirika la MIsaada la Kanisa Katoliki Italia limekwishachangia jumla ya Euro 1000, 000 kusaidia wananchi wa Ufilippini.







All the contents on this site are copyrighted ©.