Zaidi ya watu 300 wanasadikiwa kufariki dunia nchini Somalia mwishoni mwa juma kutokana
na mvua kubwa iliyonyeesha katika mkoa wa Puntland, Kaskazini Mashariki wa Somalia,
lakini jambo la kusikitisha ni kuona kwamba, vyombo vingi vya habari haviguswa na
maafa haya kana kwamba, hakuna kitu chochote kilichotokea.
Baadhi ya watu
wanasema, hii ni kutokana na mazoea, vifo vya watu nchini Somalia linaonekana kuwa
ni jambo la kawaida, lakini haipaswi kuwa hivi! Maisha ya mtu ni zawadi kutoka kwa
Mwenyezi Mungu. Taarifa zinaonesha kwamba, kuna idadi kubwa ya watu ambao hawajulikani
waliko na inahofiwa kwamba, pengine wamekufa maji. Mafuriko haya yamesababisha maafa
makubwa ambayo pengine yamemezwa na habari za kusikitisha za tufani iliyopiga nchini
Ufilippini.