Tamko la Familia ya Mungu Tanzania katika kufunga Mwaka wa Imani, Mjini Bagamoyo
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Jumapili iliyopita, tarehe 10 Novemba 2013 limefunga
rasmi Mwaka wa Imani kwa kutoa Tamko la Familia ya Mungu baada ya hija ya kitaifa
iliyofanyika mjini Bagamoyo kuanzia tarehe 8 hadi tarehe 10 Novemba 2013.
Katika tamko
lao, wamefafanua maana, malengo na utekelezaji wa Maadhimisho ya Mwaka wa Imani nchini
Tanzania. Makundi mbali mbali yametoa maazimio yanayopaswa kutekelezwa na Familia
ya Mungu nchini Tanzania, ili iweze kuwa ni chumvi na mwanga wa dunia. Tamko la Familia
ya Mungu nchini Tanzania limesomwa na Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Rais wa Baraza
la Maaskofu Katoliki Tanzania.