Papa asema, ni dhambi kubwa kuwa mfadhili wa Kanisa kwa kuiibia serikali. Kufanya
hivyo ni kuvaa sura mbili na hivyo ni kuwa kinyume na maisha ya Kikristu.
Papa
amekemea wanaotoa msaada Kanisani kwa kutaka waonekanani Wakristu wema kwa kutumia
fedha batili. Amesema, hakuna rushwa wala maisha bandia ya kujifanya kuwa Mkristu
mwema lakini kumbe ni mtu wa hatari anayeliletea uchungu mkali Kanisa, yanayoweza
kusafisha dhambi hiyo ya rushwa. Papa Francisko alieleza wakati wa Ibada ya Misa
, mapema asubuhi katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta
Alisema ni kweli sisi
sote tuna dhambi, lakini ni lazima kujilinda dhidi ya Rushwa na ulaghai. Na hasa
hatari ya kutaka kujionyesha kuwa ni muumini safi , mwenye kutoa msaada kwa kanisa
na wahitaji kwa kutumia fedha ya wizi. Kuwaibia wengine, iwe kwa mtu binafsi au serikai
au taasisi, na kutumia fdha hiyo kutoa msaada kwa kanisa . Papa anasema kufanya huko
si haki, ni sawa na yule anayotoa rushwa ili ahudumiwe, huko ni kuvaa sura mbili
katika maisha, ikiwa tofauti na maisha ya Mkristu aminifu.
Papa aliyarejea
masomo ya siku ambamo katika Injili, Yesu anatutaka kuwa na moyo wa kusamehe wanao
tukosea hata mara saba kwa siku, na kamwe bila kuchoka, inatuonyesha Yeye mwenyewe
Yesu asivyochoka kutusamehe pale tunapotubu kwa dhati dhambi zetu. Wakati Yesu
anatutaka kusamehe mara saba kwa siku , alibaini Papa , tunaiona huruma ya Mungu kwa
wakosaji. Lakini pia kifungu hiki cha Injili Yesu anakanya kwa nguvu dhidi ya
kuwa watu wachochezi na wazabina zabina na wala rushwa wanaokwaza wengine na kusababisha
dhambi.Yesu, alismea, kuliko kumkwaza mmoja wa wadogo hawa, heri mtu huyo afungwwe
jiwa la kusagia shingoni na kutupwa baharini. Maneno haya ya Yesu yanatuonyesha jinsi
ilivyo vibaya, kuwapotosha watu wengine katika njia za ukweli na aminifu . Papa alieleza
na kuhoji, tofauti kati ya dhambi na rushwa. Papa alifafanua, tofauti ni kwamba
mwenye dhambi huyaona makosa yake na kutubu na kuomba msamaha, akijisikia kuwa mnyonge
, anajisikia kuwa mtoto wa Mungu, na anajinyenyekesha , na kuomba msamaha kwa Yesu.
Lakini
kwa mtoa rushwa ,asiyetaka kutubu badala yake anatoa fedha za wizi kanisani ili aonekane
mristu safi, huendelea kuishi katika dhambi ya kujifanya kuwa Mkristo mwema na
kumbe anasura nyingine katika maisha ya kawaida yenye kusababisha madhara makubwa
na mbaya kwa wengine. Papa alimwelezea mtu wa aina hiyo , mwenye sura mbili,
anapo pambana na vikwazo vya kanisa husema, lakini , mimi ni mfadhili wa Kanisa !
Mimi kwa mkono wangu, natoa zaka na msaada kwa kanisa. Na kumbe kwa upande mwingine,
ni mwizi, mwizi anayeibia watu maskini. Haya ni madhulumu makubwa, ambayo Yesu anasema,
heri kufungiwa jiwe la kusagia shingoni na kuzamishwa baharini. Hapa Yesu hataji
msamaha kwa watu kama haolakini anatoa hukumu.
Hivyo tunaona tofauti za dhambi
na rushwa . Papa anaasa kila anaye endesha maisha kwa sura mbili, ni mwovu. Lakini
mtu anayetambua makosa yake na kumwendea Bwana kwa unyenyekevu na uchachi na kuomba
msamaha kwa Bwana anaye mpenda kw moyo wa dhati, husamehewa, na Bwana huandamana
pamoja naye .
Papa ametaja watu wenye maisha ya sura mbili, ni lazima watambue
kwamba ni sawa na uzuri wa makaburi yaliyopakaliwa rangi nje lakini ndani yamejaa
mifupa ya wafu na uozo. Na Mkristo anayedai kuwa Mkristo, lakini maisha ya si ya
Kikristu , ni mtu mwovu, anayetoa rushwa kwa kanisa ili aonekana kwa nje kuwa mtu
mwema kumbe sivyo. Papa alikamilisha homilia yake kwa kumwomba Bwana, neema ya
Roho Mtakatifu yenye kuwa na uwezo wa kuufunga uovu na udanganyifu wote, kuomba neema
ya kutambua kuwa sisi ni wenye dhambi, na hatutakatifushwi kwa kutoa rushwa , lakini
kwa kukutana na Bwana katika sakramenti ya kitubio.